Saturday, May 20, 2017

Cleveland Cavaliers vs Boston Celtics - Full Game Highlights | Game 2 | May 19, 2017 | NBA Playoffs



Cleveland Cavaliers vs Boston Celtics - Full Game Highlights | Game 2 | May 19, 2017 | NBA Playoffs
- Like & Share if you like this video! If you dislike, please comment suggestions for
 improvement next videos.
- For live streaming and NBA news, go to NBA.com and subscribe to NBA
League Pass: nba.com/leaguepass

Movie inayozungumzia maisha ya ‘Whitney Houston – Can I Be Me’



Wakiwa katika maandalizi wa kuandaa 'documentary' inayozungumzia maisha halisi ya
Whitney Houston inayokwenda kwa jina la  ‘Can I Be Me’, ambayo itakuwa ikielezea
maisha halisi ya mwanamuziki huyu ambayo wengi walikuwa hawahajui na sauti
yake ya dhahabu.

floydmayweather ameonyesha Rolls Royce zake

Kijana mwenye fujo floydmayweather ameonyesha Rolls Royce zake
 

Pia anakukaribisha kiwanja chake kipya cha girlcollection

A post shared by Floyd Mayweather (@floydmayweather) on





‘Sipendi wanaume wafupi’ -Shilole



MSANII wa Bongo Fleva, Shilole ameamua kutaja sifa za mwanaume anayempenda na kusema kuwa anavutiwa sana na wanaume warefu kuliko wafupi.
Shilole anasema mesema anampenda mwanaume yoyote yule anaejitambua ingawaje kidogo sifa za nje awe mrefu kwani hana hisia zozote kwa mwanaume mfupi.
“Napenda mwanaume yoyote yule ilimradi anajitambua basi, suala la muonekano hilo linatengenezwa ila kiukweli kabisa napenda sana mwanaume mrefu, mwanaume mfupi kwangu hapana.
“Sipendi wanaume wafupi, Barnaba yeye ni mfupi na kila mmoja ameumbwa na Mungu tofauti. Ila sasa hivi vigezo na masharti kuzingatiwa,”anasema Shilole.
Anaongeza kwa sasa anatamani sana kuolewa kwani ndoa ni heshima kwa mwanamke .
“Hamna mtu asiyependa kuolewa, ndoa ni heshima ndiyo maana unasikia watu wanasema mke wa fulani yule, muwe wa fulani yule lakini siyo aah yule si mwanamke tu kwa hiyo ndoa ni heshima” anasema Shilole.

Shamsa Ford awapa somo mastaa wa kike


MWIGIZAJI wa filamu nchini Shamsa Ford amewabwatukia mastaa wa wanawake waache tabia za kuchagua wanaume wa kuwaoa, kwani leo wana majina makubwa na wanaonekana warembo lakini ipo siku itafika hata hao wanaume wanaowatongoza leo watapotea kabisa.
Akizungumza wiki hii, Shamsa Ford anasema kwa sasa wanawake wenye majina makubwa wanajiona warembo kiasi hufikia hatua hata ya kusubiri wanaume matajiri wa kuwaoa bila kukumbuka kuwa hata hao matajiri wana watu wao.
“Wasichana wenzangu maisha ni mafupi , leo tunavuma na kupendwa kila kona tunapokatiza ila kuna muda utafika hata nzi hakusogelei.Hata uwe mzuri na maarufu kiasi gani lakini ndoa ina heshima yake.
“Msiwe wachaguzi sana, maana ukisema unamsubili tajiri aje akuoe na yeye huyo tajiri ana mwanamke wake aliyetoka naye mbali kimaisha,”anasema Shamsa kwenye ukurasa wake wa Instagram,”anasema.
Anafafanua ni muhimu kumuomba Mungu akupe mwanaume mwenye kumjua Mungu, mwenye upendo, heshima, mtafutaji hayo mengine yanakuja tu. Nguvu ya mmoja ni tofauti na ya wawili,”anasema.Shamsa Ford kwa sasa yupo kwenye ndoa na mfanyabiashara Chidi Mapenzi.

Amber Rose anusurika na msala wa Kibaka



KICHUDA mwenye kismati cha kutoka na Masupastaa nchini Marekani, Amber Rose amesema anahisi kuna mtu alimvamia nyumbani kwake na kulala Zaidi ya masaa manne.
Inasemekana nyumba ya Amber iliyopo maeneo ya San Fernando Valley ilivamiwa na kibaka huyo siku ya Jumatano ambapo alipitia dirishani maeneo ya jikoni kabla ya kuzama katika vyumba vya nyumba hiyo.
Amber ambaye anaishi na mwanae aliyezaa na Rapa, Wiz Khalifa na Mama yake aliwapigia simu Polisi ambao walifika katika eneo la tukio na kufanya uchunguzi wa tukio hilo licha ya kubaini kutoibiwa kitu chochote.

DJ Khaled Surprises UC Berkeley Graduates



On Thursday (May 18), the super-producer surprised statistics graduates at the University of California, Berkeley, when he popped up to perform his triumphant anthem “All I Do Is Win.”
The performance, which followed entrepreneur Steve Stoute’s commencement address, was accompanied by a speech from Khaled.

“I didn’t come out here to do a concert,” he said. “I came to praise the young kings and queens for graduating today. This is amazing. I ain’t graduate myself, so this is the closest thing to graduating for me too.”
But of course, Khaled didn’t leave without dropping some major keys for the graduating class. “This is so inspiring and such a motivational situation today,” he said. “They didn’t believe in me at one time in my lifetime, but I had to bet on myself and look at me now. I’m on the stage with young kings and queens and the generation of geniuses that’s gonna run the world…They don’t want us to graduate, so we gon’ graduate!”

Afterwards, Khaled celebrated the occasion with a post on social media. “Thank you @stevestoute for bringing me out at your commencement speech for UC Berkeley Statistics Graduates,” he wrote. “Congrats to the young world the world is yours @nas voice!”
After topping the charts and going gold with his Justin Bieber, Quavo, Lil Wayne, and Chance the Rapper-assisted “I’m the One,” Khaled is prepping the release of Grateful, the follow-up to last year’s Major Key.

 

NYIMBO INAYOSUMBUA ARUSHA KWASASA.- NYIMBO BORA YA HIP HOP 2017


NYIMBO BORA YA HIP HOP 2017 Kutoka kwa yule yule rapa machachari anayesumbua mitaa na album yake ya kifo cha bongo fleva sasa ameachia nyimbo gumzo Arusha nzima kila mtu kasema huu ndio wimbo bora wa mwaka wa HIP HOP kutoka ArushaPAKUA HAPA http://bit.ly/2mUzAjh HAINA UBISHI DIRT VERSION PAKUA HAPA http://bit.ly/2mmQTMX PAKUA ALBUM NZIMA YA KIFO CHA BONGO FLEVA ARUSHA HAPA http://bit.ly/2inPUYz



Celebrity Style: Jada Pinkett, Pharrell Williams, Evan Ross, Harry Styles, A$AP Rocky, Russell Westbrook


Music mogul Pharrell Williams attended TechCrunch Disrupt event wearing a 
Thom Browne nautical embroidered navy blazer ($2,900). The Navy blue wool jacket features multiple marine life embroideries. This jacket is also available in grey wool blend.
Photo: Getty Images

navy blazer
Actress Jada Pinkett Smith was spotted in Beverly Hills, wearing a Gucci 
butterfly bomber jacket, Adidas Originals sneakers, and carrying a black Hermes wallet.

Jada Pinkett

Power couple Evan Ross and Ashlee Simpson were seen leaving dinner at TAO 
restaurant in Hollywood. Evan wore a Saint Laurent palladium black velvet jacket 
and John Varvatos velvet fleetwood lace boots ($698).
jacket
Photographer Group / Splash News
boots

Rapper A$AP Rocky was spotted leaving The Peppermint Club in West Hollywood, wearing a vintage varsity jacket, Martine Rose logo white t-shirt, Valentino pants, and Air Jordan retro 1 sneakers in red and black color way.
Photo: Splash News Online

One Direction star Harry Styles was spotted at the BBC One Show in London, 
wearing a custom Harry Lambert bomber jacket, Saint Laurent jeans, and Saint Laurent boots.
t shirt

Moji Olaiya afariki dunia


MSANII wa filamu za Nollywood, Moji Olaiya, 42 amefariki Dunia juzi baada ya  kujifungua kwa shida akiwa hospitalini nchini Canada.
Kifo cha msanii huyo ni pigo kwa Nollywood kutokana na umuhimu wake wake hasa katika filamu za Yoruba.
Moji ambaye alimkaribisha mtoto wake mpya Machi, mwaka huu, alifariki juzi usiku nchini humo.Taarifa zilieleza alifariki baada ya kupata ugonjwa wa shambulio la moyo.
Tasnia hiyo imekuwa kwenye huzuni mkubwa tangu kufariki kwa mwanamama huyo ambaye alikuwa na msaada mkubwa ka wasanii wanaochipukia.


Chioma afurahia kuwa bibi

MSANII nyota wa Nollywood, Chioma Chukwuka, ameonesha furaha ya kipekee kwa kuzaliwa mpya wake huku akijisifia amepata mjukuu.
Tangu kufariki kwa mama wa msanii huyo, Grace Egoyibo Chukwuka, mtoto wake wa kwanza, aliamua kumfanya kama ndiye mama yake kwa mujibu wa utamaduni wa Igbo.
Katika ukurasa wake wa Instagram aliandika:”Kwa leo nampa utukufu wake Mungu! Nimekuwa bibi tena”.

Nyota 10 wa kike wanaopendwa Nollywood hawa hapa


TAASISI ya Ushauri ya NOI Global, imefanya uchunguzi na kutaja wasanii nyota 10 wa kike nchini hapa wanaopendwa zaidi katika tasnia hiyo.
Uchunguzi huo ulifanywa kwa kuwakusanya wadau mbalimbali wa filamu na kuwapigia kura wasanii wanaowaona wanapendwa.
Kwa mujibu wa matokeo ya uchunguzi huo, wadau wengi walisema wanafurahia kuangalia zaidi filamu za Nollywood kuliko vitu vingine.
Asilimia 39 wanapenda kuangalia filamu za mapenzi za kuchekesha, asilimia 40 vichekesho na asilimia 14 wanapenda filamu za mapenzi tu.
Ilielezwa filamu itapendwa zaidi endapo mshiriki atakuwa msanii wa kike au kuume ambaye ni maarufu katika jamii.
Pamoja na hali hiyo lakini wengi wa walioulizwa walisema asilimia 48 ya Wanaigeria wanapenda kuangalia filamu za Nollywood ila wanapaswa kuboresha utunzi wao.
Wasanii hao 10 waliotajwa katika uchunguzi huo ni Genevieve Nnaji, Mercy Johnson, Omotola Jalade, Funke Akindele, Ini Edo, Patience Ozokwor, Mercy Aigbe, Stephanie Okereke, Chika Ike na Fathia Balogun.

Wasanii waungana kupinga unyanyasaji wanawake, watoto

Mercy Johnson-Okojie
WASANII nyota wa filamu nchini hapa (Nollywood), wameunga mkono kampeni maalumu iliyowekwa na Serikali kupinga vitendo vya unyanyasaji kwa wanawake na watoto.
Mratibu wa muunganiko huo wa nyota hao, Uche Ogbodo, ambaye amekuwa mstari wa mbele kusapoti kampeni hiyo, anasema tayari nyota kama Mercy Johnson-Okojie, Chioma Akpotha, Uche Jombo, Omoni Oboli, Stephanie Linus, Annie Idibia ni baadhi ya wasanii ambao wameonesha sapoti ya wazi.
Kwa mujibu wa mratibu huyo, kampeni hiyo itatoa thamani halisi ya wanawake na watoto. “Kupitia kampeni hii tunaimani tutawaelewesha Waafrika kwamba wanawake na watoto wanapaswa kuhudumiwa kwa uangalifu na upendo,” alisema Ogbodo.
Wasanii wengine ambao watajiunga katika kampeni hiyo ni pamoja na Halima Abubakar, Omotola, Yvonne Okoro, Kate Henshaw na Lilian Esoro.

Mr Blue ni alama ya mlima uliosimama bila kudondoka


UNAFUNGUA redio unakutana na rekodi ya kibabe ya baki na mimi, unageukia runinga yako unauona wimbo wa mboga saba ambao huwezi kudhani kama msanii aliyeuimba ana miaka 13 kwenye muziki wa Bongo Fleva, pumzi inakushuka tabasamu lazima lijengeke usoni.
Miaka 13 nyuma wakati muziki wa kuimba ukiwa umeanza kushika kasi, mashabiki wanampokea msanii ambaye pengine alitoka akiwa na umri mdogo kuliko waliokuwepo, sura ya kitoto, umbo dogo tena ikisemekana alikuwa mwanafunzi wa kidato cha kwanza pale Benjamin Mkapa Sekondari,

Kariakoo! ni nani?.
Heri Samir ‘Mr Blue’ alikuwa ameingia katika tasnia ambayo awali watu walikuwa wakiichukulia poa, hakuna ambaye aliuona muziki kama biashara na hata utokaji wake kwa maana ya kurekodi na kutoka kisanii ilikuwa changamoto zisizo na maelezo mazuri ya kusimulia.
Ungeweza kutembea kwa miguu kutoka Temeke mpaka Masaki kwa Master Jay kurekodi au ungewahi mapema kwa P Funk na bado akakuzingua kuingia studio, kwa umri wake angemudu vipi, angeweza kustahimili kwa kipindi kirefu?.
Haikua hivyo tu alitoka katika nyakati ambazo muziki wa Hip Hop ulikuwa katika kilele chake, nani angekusikiliza wewe unaeimba? Waliofanya muziki huo waliitwa wabana pua, mabishoo na majina mengine ya kuudhi, changamoto zilikuwa nyingi nani amesahau ile stori ya ‘kijinga’ kuhusu Blue na Kalapina? Tuachane na hayo, muda umepita!

Kuanzia siku ile aliyoachia wimbo wake wa Blue blue mpaka leo hajawahi kushuka kisanii, hajawahi kupanda pia juu kwa kiwango kikubwa ameendelea kuwepo palepale, kuna wengi aliwakuta kwenye gemu wameshindwa wamekaa pembeni lakini yeye bado yupo.
Wapo waliomkuta yeye tena wakatengeneza majina yao kwa kiwango cha ajabu kumshinda lakini wakakosa muendelezo mzuri ‘consistency’ wakaanguka na mpaka sasa wameshindwa kunyanyuka, yeye bado yupo tena akiachia ngoma kila kukicha zenye ujazo na uwezo wa kutawala redio zote, huo tunauita ufanisi wa hali ya juu!

Kuna utofauti mkubwa kutoka kwa Blue wa Blue blue na kiss kiss na yule wa Tabasamu hadi kwa huyu wa Baki na mimi na Mboga saba, ipo tena sio ndogo, kuanzia muonekano wake mpaka staili ya muziki anaoufanya, twende taratibu!
Jaribu kuwasikiliza wasanii wengi wa Hip Hop staili waliyoanza nayo ya kurap wapo walioanza kuikimbia, msikilize Darasa huyu wa muziki sio yule wa sikati tamaa, Joh Makin wa Hao sio huyu wa Nusu nusu.

Wengi wamelegeza ‘floo’ wapo walioamua kuimba kabisa na kuachana na kurap, Kalapina na ugumu wake alifanya hivyo lakini hali haipo hivyo kwa Blue yeye alitoka kwenye ‘kubana pua’ na kuanza kurap na amewashika mashabiki kwa muda mrefu bila kushuka.
Jaribu kuhudhuria shoo zake utagundua ni moja kati ya wasanii wa muda mrefu ambao wanaweza kumiliki jukwaa kwa muda mrefu bila kuchoka huku akiwarukisha kwata mashabiki kwa namna atakavyo yeye, kwanini ashindwe wakati anaishi mioyoni mwao?.

Atashishindwa vipi ilihali nyimbo alizonazo hazijawahi kuboa nyoyo za wale wanaolipa viingilio vyao kwenda kumtazama? Maonesho makubwa yamekuwa yakitoa majibu kuhusu ubora wake, hakamatiki.

Sio kila msanii anaweza kudumu kwenye huu muziki kwa muda mrefu bila kushuka, pengine Dully Sykes anaweza kushikilia rekodi hiyo kwa sasa lakini Blue ni mmoja wa wale ambao wameutendea haki muziki huu, uwezo wake wa kuachia ngoma zinazoweza kusumbua hadi kwenye bodaboda ndio unaomfanya akubalike kila siku na kuzidi kuwepo hapo alipo kwa muda mrefu.

Kipindi Fulani aliwahi kukabiliwa na skendo za utumiaji wa madawa ya kulevya ‘unga’ sawa! Inawezekana kweli aliwahi kutumia, alikula au alivuta sina uhakika lakini aliwahi kutokeza hadharani na kukiri kwamba alikua akivuta bangi na sigara na sio unga, umejifunza nini hapo?
Uthubutu! Alitambua kuwa tayari kuna kengele ya hatari imegota kichwani mwake, kwamba mashabiki washaanza kumhisi vibaya na alitambua athari ya kuwa na skendo mbaya masikioni mwa mashabiki, angedondoka! Angesahaulika haraka! Angepotea.

Ni nani amewahi kuwa na skendo za utumiaji madawa akabaki salama? Langa? Mungu amlaze mahali pema lakini ‘unga’ ulimuaribia, Chillah je? Sote tunafahamu kiasi gani anapambana kurudia kilele chake.
kwa miaka ya karibuni Chid benz ni mfano ulio hai, kwanini yeye aendelee kuwepo huko? Machale yalimcheza!

Wiki iliyopita nilikuwa niliandika namna ambavyo wakongwe kwenye gemu wanavyopigishwa kwata kwa sababu wameshindwa kumudu kasi ya vijana wa sasa.
Wanaishia kuweka chuki na wivu inayopelekea kuingia shimoni Zaidi, lakini kwa Blue hali siyo hivyo bado ameendelea kuishi kama ‘underground’ na hiyo imezidi kumzidishia heshima yake.

Miezi michache iliyopita ilisemekana aliingia katika mikwaruzano ya kugombea jina yeye na Diamond, eti wote wanajiita Simba lakini nani ambaye angeweza kukaa kimya bila kurushiana maneno na msanii ambaye kwa sasa amelishika soko?

Wengi wanafanya hivyo wakiamini kuwa wanajizidishia umaarufu lakini kwa Blue hali haikua hivyo alitulia kimya na ghafla bifu likaisha, hiyo tunaita busara za mkongwe, yaani kwa hadhi na heshima aliyonayo kwenye muziki ingekua kichekesho kuingia katika ugomvi na ‘dogo’,.


Sio hilo tu hata ugomvi wake na Sugu uliisha vizuri katika masikio ya mashabiki hata kama moyoni wanaendelea nao lakini kutoendeleza chokochoko nayo ilikua heshima kwake.
Blue ni mfano katika gemu ni kisiki kilichoshindwa kukatika kirahisi na bado ameendelea kuotesha mizizi yake, pengine tabasamu ndio rekodi iliyonogesha Zaidi umwamba wake, achilia mbali namna alivyowafanya ‘kitu mbaya’ Dully na Joslin kule kwenye Dhahabu.

Diamond, AY wanastahili heshima

KILA unapotaka kuzungumzia mafanikio ya muziki wa Bongo Fleva katika ngazi ya kimataifa, huwezi kuepuka kutaja majina ya hawa wasanii wawili.
Diamond Platnumz akiwakilisha ngome yake (lebo) ya Wasafi Classic Baby (WCB), huku kipindi cha nyuma AY akiibeba kambi yake ya Unit Entertainment.
Wamekuwa wakipambana sana kuhakikisha muziki huu unafika mbali zaidi na kupata dhamani kubwa kwenye mataifa mengine, na hilo wamefanikiwa kwa asilimia kubwa.
Leo katika safu hii pendwa ëZeze kolaboí, wewe msomaji wangu nakuchambulia jinsi Diamond na AY alivyofanikiwa kupeleka     Bongo Fleva kimataifa kwa kufanya kolabo na wasanii wa nje.
 
Tuanzie Nigeria
Kama kumbukumbu zangu zipo sawa, AY ndiye msanii wa kwanza kutoka kwenye Bongo Fleva kufanya kolabo kubwa na wasanii kutoka Nigeria.
Mwaka 2008 wakati kundi la P Square linafanya vizuri na nyimbo zake kama Temptation na Dome  walikuja Tanzania kufanya ‘show’ , ndipo AY alipoona kuna uwezekana wa kufanyao nao kazi.
Bila kupoteza muda wakaingia studio B Hit’s kwa Prodyuza Hermy B na kutoa wimbo uliokwenda kwa jina ‘Freeze’ ambao ulishangaza wengi na kujiuliza AY amewezaje!
Weka nukta hapo, msanii wa kwanza wa Nigeria kupewa shavu na Diamond ni Davido, ambaye mwaka 2013 kwa pamoja walitoa wimbo uitwao ‘My number one’ uliyomleta Diamond mpya kwenye Bongo Fleva.
Kazi ilifanyika studio za Burn Records kwa prodyuza Shed Clever, licha ya wimbo huu kumtambulisha Diamond kimataifa, pia ulimtambulisha Shed Clever   na kumuwezesha kuwania tuzo ya Afrimma Dalas Texas Marekani.
 
Unapaswa kujua na hili
AY hakuishia kwa P Square tu, bali alikuja kufanya kazi na wasanii kama Goldie Harvey wimbo uliitwa ‘Skibobo’ uliyotoka mwaka 2012.
Goldie Harvey alikuwa mwakilishi wa Nigeria katika shindano la Big Brother Africa (BBA) kwa mwaka 2012, ambapo alianzisha uhusino na msanii wa Kenya Prezzo, kwa mapenzi ya Mwenyenzi Mungu mwaka 2013 alifariki dunia.
Weka nukta hapo, Kama hiyo haitoshi mwaka 2013 AY pamoja na Mwana FA walimpa shavu J Martins kwenye wimbo uitwao ‘Cheza bila kukunja goti’, chini ya prodyuza Marco Chali.
Diamond nae alizidisha mashambulizi kwa kufanya kazi na wasanii kama Iyanya aliyempa shavu kwenye wimbo wa ëBum bumí uliyotoka mwaka 2014. Pia Mr Flavour alichukua nafasi kwa kupewa shavu kwenye wimbo wa Nana uliopikwa na prodyuza Nahreel.
Ili kudhibitisha ubora wake, mwaka mwaka jana amedondosha ngoma aliyowashirikisha P Square, wimbo unaitwa Kidog’, ambao unabamba hadi sasa.
 
Hadi Marekani
Diamond na AY si watu wa mchezo kabisa, wote wawili wanaingia katika vitabu vya kumbukumbu kwa kufanya kazi na wasanii wa Marekani.
AY alianza kwa kumshirikisha miss Trinity kwenye wimbo uitwao Good Look  uliotoka mwaka 2011.
Mwaka 2014 aliachia nyimbo mbili kwa mpingo ambazo alifanya na wasanii wa Marekani.
AY alimshirikisha Sea Kingston kwenye wimbo uitwao Touch me. Pia alimshiriksha tena miss Trinity na Lamiya kwenye wimbo uitwao ëItís going downí.
Video ya wimbo huu ilifanya Marekani, AY anakiri ni moja ya video alizowekeza fedha nyingi zaidi. Tukihamia kwa upande wa Diamond, wimbo aliofanya na msanii wa Marekani ni Marry You ambao amemshirikisha Ne-Y, msanii aliyetamba na nyimbo kama, So Sick na Miss Independent.
Wimbo huo ‘umepikwa’ na prodyuza Shed Clever, na iliwalazimu kusafiri hadi Nairobi Kenya wakati Neyo alipokuwa anafanya ‘show’ huko ili kukamisha kolabo hiyo.
 
Pindi walipokutana
AY alimpa shavu Diamond kwenye remix ya wimbo wa Zigo ambao ulisumbua sana wakati ulipotoka.
AY anasema kama asingempata Diamond katika wimbo huu, basi angemshirikisha msanii Wizkid kutoka Nigeria.Kwa kujiamini AY anasema imefika wakati kwa wasanii wa Tanzania kutengeneza muziki mkubwa bila kushirikisha wasanii wa nje.
Hilo wamefanikiwa kwa asilimia kubwa kwa kuwa tuliona wimbo huu ukifanya vizuri na kuingia katika chati za muziki za vituo vikubwa vya televisheni vya Afrika na Ulaya pia.
Video ya wimbo huu hadi sasa katika mtando wa Youtube umetazamwa na watu zaidi ya milioni 8.8 tangu utoke Januari 22 mwaka jana.
Tumalize hivi, kutambua ukubwa wa hii kolabo AY anawakutanisha maprodyuza watatu ambao ni Nahreel, Marco Chali na Hermy B kunogesha mdundo wake.
Peter Akaro
Kwa maoni 0755 299 596

Pregnant Beyonce Shares Super Sweet Snaps From Mother’s Day


Beyonce, who is on the brink of becoming a mother of three, celebrated Mother’s Day
in style last week.
A post shared by Beyoncé (@beyonce) on

In her tried and true practice of giving a retrospective look at her life, Queen Bey has today shared snaps from the occasion with daughter Blue Ivy, mom Tina Knowles, and husband Jay Z.
The group soaked in all the sweetness of the Museum of Ice Cream in Los Angeles.
Peep more pics of Bey, who is due to give birth to twins imminently, and her crew below..


Celebrity Style: Rihanna, Bella Hadid Stun at Cannes Film Festival




Pop singer Rihanna and model Bella Hadid turned heads at the ‘Okja’ Cannes Film Festival premiere in Cannes, France on Friday. Rihanna accessorized her white floor length gown with emeralds from her Chopard jewelry line.
Photos by Andreas Rentz/Getty Images


Model Bella Hadid attended the premiere wearing a quilted red gown from the Christian Dior Spring 2017 Couture Collection.





Rihanna