Tuesday, January 3, 2012

NEW SONG 2012, C-SIR MADINI - NISHIKE MKONO



Heri ya mwaka mpya mdau,

Tetemesha Recordz inayo furaha kuuanza mwaka 2012 kwa kutambulisha wimbo mpya wa C-SIR MADINI unaitwa NISHIKE MKONO. Wimbo huu ni mwendelezo wa love story ya wimbo uliopita wa C-SIR unaoitwa KIFUNGO HURU. Video ya NISHIKE MKONO itafuata baadae. Thanx for ur support na tunaamini utaendelea na moyo huo na sisi tunaahidi kuendelea kufanya kazi bora.

CREDITS

Track Name: NISHIKE MKONO

Artist: C-SIR MADINI

lyrics composed by: C-SIR MADINI & KID BWOY

arranged by: C-SIR MADINI

Produced by: KID BWOY

Mixed by: KID BWOY

Studio: TETEMESHA RECORDZ

JANUARY 2012

contacts: C-sir Madini +255 712 719004

cheers

--
Sandu G. (Kid bwoy)
CEO/Executive Producer
Tetemesha Entertainment
e-mail:
tetemesharecords@gmail.com
Dar es salaam,
Tanzania,
East Africa
.


Lyrics:-

"NISHIKE MKONO" LYRICS by C-SIR MADINI

E:\tetemesha-new.jpg

Track Name: NISHIKE MKONO

Artist: C-SIR MADINI

lyrics composed by: C-SIR MADINI & KID BWOY

arranged by: C-SIR MADINI

Produced by: KID BWOY

Mixed by: KID BWOY

Studio: TETEMESHA RECORDZ

JANUARY 2012

Intro:

Uuuuuh, uuuuuh, uuuuuuuh

Usiniache nyuma aaah, we nishike mkonooo uuuh

VERSE 1:

Nisharudisha moyo wangu nyuma japo mwanzo niliachwa dilemma,

Nikajiuliza nitapata wapi mwingine wa kunipoza mtima,

Kumbe, kumbe sangara na pweza kuna tofauti,

Kumbe, kumbe sangara na pweza kuna tofauti,

Nilitabika jangwani na wewe maji ulikuwa wapi,

Nilitabika juani kivuli changu ulikuwa wapi,

Sina budi kusema asante asante asante mola,

Sina budi kusema asante asante weweee

CHORUS:

Twende nishike mkono usiniache nyuma tena,

Kwani we ndio chaguo langu usiniache nyuma tena,

Twende nishike mkono usiniache nyuma tena,

Kwani we ndio chaguo langu usiniache nyuma tena,

VERSE 2:

Kibatari huzima mapema yanapokwisha mafuta mamama,
pendo langu ndio pete yangu ntakuzunguka wewe mamama,

Hata barabara ndefu vipi huwa haikosi kona ah ah,

Nipende nikupende endapo nitakuudhi nitakuomba msamaha ihe ihe,

Mapendo mapendo haa, mapendo mapendo maa,

mapendo mapendo haa, mapendo mapendo maa,

Wangu mola namshukuruku kukuweka chini ya jua

Wangu mola namshukuruku kukuweka chini ya jua

CHORUS:

Twende nishike mkono usiniache nyuma tena,

Kwani we ndio chaguo langu usiniache nyuma tena,

Twende nishike mkono usiniache nyuma tena,

Kwani we ndio chaguo langu usiniache nyuma tena,

Verse 3:

Ndege iliyonibeba mie mwanzoni, sikudhani kama ingenitupa

Nakutegemea parachuti wangu, niongoze mpaka tutapofika,

Nakuahaidi ntakirimia, kwa chochote ntachopata,

Nakuahidi sitokimbia, funguo za pingu zishapotea,

Mi ni mmea nishaota kwako ooh, kustawi kwako sigomi,

Nachohitaji uangalizi wako ooh, jua maneno maneno hayajengi

CHORUS:

Twende nishike mkono usiniache nyuma tena,

Kwani we ndio chaguo langu usiniache nyuma tena,

Twende nishike mkono usiniache nyuma tena,

Kwani we ndio chaguo langu usiniache nyuma tena,

Outro:

Ni C-sir madini (tena), sitaki kumulika mwizi (tena),

Sitaki sumu ya penzi (tena),sitegemei kulia(tena),

Wala sitaki kuumizwa (tena), sitaki mwenye kigeugeu (tena),

Nasema sitaki vigeugeu (tena),, Tetetetemeshaaaaaaa


0 Comments: