Tuesday, August 22, 2017

Van Vicker, mkewe waponda raha Marekani

HIVI unajua kuwa ‘playboy’ Van Vicker kaoa! Ukweli ndio huo, nyota huyo anayependwa na wadada wengi Nollywood, ameoa na hivi sasa anakula bata Las Vegas, Marekani.
Msanii huyo anayetokea Ghana amemuoa Adjoa Van Vicker ambaye tayari amemzalia watoto watatu.
Pamoja na vituko vyake vya kisanii, nyota huyo kumbe alioa miaka 14 iliyopita lakini kitu cha kushangaza wawili hao wapo pamoja wakila raha kwa miaka 23 sasa.
Van Vicker ambaye amefikisha miaka 40 ilipofika Agosti Mosi, alitumia muda wake na mkewe huyo aliyedumu naye miaka 14 jijini Las Vegas.
Katika kuthibitisha hilo, nyota huyo aliweka picha katika mtandao wake wa Instagram akijaribu kumbusu mkewe huyo.

0 Comments: