Saturday, July 15, 2017

Lil Kim kumaliza ugomvi kati ya Remy Ma, Nick Minaj


RAPA wa kike nchini Marekani, Lil Kim wakati wa kusherehekea siku yake ya kuzaliwa moja ya mambo yanayokumbwa ni maneno yake ya kujiweka mbali na bifu kubwa linalofuatiliwa na watu wengi nchini humo.

Bifu la Nicki Minaj na Remy Ma lilizidi kuwa kubwa baada ya Remy Ma kutwaa tuzo ya BET BEST FEMALE RAPPER  lakini licha ya bifu lao kuwa kubwa Lil Kim alishasikika katika mahojiano na kituo cha Billboard kuhusu bifu hilo ambapo amesema hana mpango wa kuungana na Remy Ma kumdiss Nicki Minaj.
Lil Kim ambaye alishamdiss NickiMinaj kupitia ngoma ya ‘Black Friday’ aliongeza hana bifu kabisa na Nicki kwa kuwa walishamaliza na kikubwa anachoweza kueleza kuhusu marapa hao wa kike ni kuwashirikisha wote wawili katika album yake mpya.

0 Comments: