Saturday, November 17, 2012

LEO AY NA CPWAA NDANI YA CHANNEL O VIDEO MUSIC AWARDS 2012


Leo usiku, ndani ya Jiji la Johannesburg, kitongoji cha Soweto, katika viwanja vya Watler Sisulu, zinafanyika kwa mara ya tisa, tuzo za video bora za muziki Afrika zinazoratibiwa na kituo cha Televisheni cha Channel O, huku Tanzania ikiwa na wawakilishi wawili wanaowania jumla ya tuzo nne.

Hii siyo mara ya kwanza kwa wanamuziki hawa kutajwa kuingia katika tunzo hizi zinazodaiwa kuwa za pili kwa ukubwa Afrika ukiachana na ile ya Kora, kumbukumbu za gazeti hili zinaonyesha mwaka jana pia wanamuziki hawa wakiwa na mwenzao wa kike Sarah Kais walikwenda huko huko Afrika ya Kusini, na kurudi wakiwa hawajaambulia hata tunzo, na katika uchunguzi wetu tukagundua kwamba kwetu hapa huwa si watendaji sana kwenye suala la kura.


Mwaka huu zimekuwapo kampeni kila kona ya nchi, za kila aina, na mpaka tamasha la kuomba kura likafanyika ili mwisho wa Tanzania nayo iingie kwenye ramani ya kimataifa ya muziki kwa kuwa na mwanamuziki aliyetukuka kutokana na sanaa yake hiyo.

AY anawania jumla ya tunzo tatu
Ya kwanza ni Most Gifted East African Video, ambapo wimbo wa I dont wanna be Alone, AY na Sauti Sol umeingia, yeye hapa anapambana na Keko akimshirikisha Madtraxx katika Make You Dance,

Camp Mulla nao wanawania tunzo hii hii kupitia wimbo Party Donít Stop, KíNaan akimshirikisha Nas katika Nothing To lose na mwisho kabisa anayewania tunzo hii ni Navio kwa kutumia wimbo wake One & Only Ya pili ni Most Gifted Video of the Year, wimbo wake Speak with your Body, AY ameshirikiana na Romeo na Lamaya. tunzo hii inawaniwa na watu 10!

Hapa wengine wanaowania tunzo hii hii ni:
DJ Zinhle Feat. Busiswa - My Name Is
Khuli Chana Feat. Notshi - Tswa daar
Toya Delazy - Pump It On
Lizha James Feat. Perola - Leva Boy
Big Nelo - Sente beat
Díbanj - Oliver Twist
Brymo - Ara
Sarkodie Feat. Obrafour - Saa Okodie No
Camp Mulla - Fresh all day

Na wimbo huo huo Speak with your Body unaingia kwenye kundi la Most Gifted male Video na hapa anapambana na Oliver Twist ya D Banj kutoka Nigeria, na Big Nelo wa Angola ambaye ameingia, Pro kutoka Afrika ya kusini na wimbo wake Makasana na wimbo wake Sente O’ Beat.

CPwaa
Yeye anawania tunzo moja ya Most Gifted Dance Video of the year” kupitia wimbo wake wa Hnmmm abapambana na DJ Zinhle akimshirikisha Busiswa katika My Name Is, DJ Cleo pia anawania tunzo hii hii na wimbo wake Facebook, OS3 kwa kushirikiana na Tchoboly kupitia wimbo Mokongo pia wamo katika kuwania tunzo hii pamoja na Davido kupitia wimbo Dami Duro pamoja na Bucie kupitia Get Over It!

Picha inaonekana wazi kwamba wanamuziki wetu wako katika wakati mgumu ukilinganisha na watu wanaoshindana nao katika tunzo hizi ingawa kila mtanzania ana matumaini kwamba safari hii inawezekana wasanii wetu wakarudi na tunzo ambazo zitasababisha sanaa ya kitanzania kuwa katika ramani nzuri kama ulivyo utalii wetu pia.

Tofauti na nchi za wenzetu, tanzania kwa upande wa sanaa, hasa ya muziki, Jiji la dar es salaam pekee linaonekana kuwa na muamko wa kusaidia wasanii katika kampeni za kimataifa za kimuziki kuliko mikoa mingine ambapo wamekuwa ni mashabiki wa kusubiri burudani tu.

AY kwa upande wake alisema,” mi nashukuru kwa watu wote walionisupport maana kusupport AY ni kusupport muziki wa Tanzania, magazeti, TV na Radio stations na blogs, mitandao ya kijamii na wote walioonyesha nia.

Nawashukuru sana,yale ni mashindano na kila mtu anavyoenda kule anaenda akiwa na moyo wa kushindana, ila ukiwa mshindani ukubali kuna kushinda na kushindwa kutokana na kura zilizopigwa so natumai watu walipiga vya kutosha. categories zote ziko tough but I believe tutafanikisha zote au moja”.
Mungu ibariki Tanzania, Mungu wabarariki wasanii hawa walete heshima kwa nchi yao
Source: Henry Mdimu 
  All the Best TeamTanzania in South Africa for CHANNEL O MUSIC VIDEO AWARDS #CHOMVA2012 

0 Comments: