Saturday, August 19, 2017

Thea asema fimbo za baba yake zimemjenga kimaadili

MWIGIZAJI wa filamu za Bongo Salome Urassa a.k.a Thea amesema anaendelea kukua kwenye maadili bora kutokana na malezi ya wazazi wake hasa baba yake aliyemuwekea misingi ya nidhamu.
Thea anasema wiki hii kuwa baba yake alihakikisha anakuwa kwenye maadili mema na anakumbuka fimbo ambazo alikuwa anakutana nazo anapofanya kosa.Hivyo zimemsadia kuwa mwadilifu.
“Baba yangu alikuwa kiboko, nilikuwa napigwa fimbo na ukubwa wangu huu, kwa hiyo niko hivi nilivyo kwa sababu ya malezi bora ya baba yangu hasa fimbo zake,”alisema Thea.

0 Comments: