Tuesday, August 22, 2017

Ruby aonja penzi la Soudy Brown... kisha kasepa

RUBY amefichua siri kuwa amewahi kutoka kimapenzi na mtangazaji wa kipindi cha Shilawadu cha Clouds FM, Soudy Brown miaka miwili iliyopita.
Hata hivyo ameeleza baadae waliachana kutokana na kubaini kuwa mmoja wao hakuwa na msimamo kwenye mapenzi.
Kwa mujibu wa mtandao wa Spin Tanzania umedai Ruby anasema Soudy  ndiye mwanaume pekee aliyetoka naye kimapenzi kutoka kwenye muziki wa kizazi kipya.
“Nikiri huko nyuma nimewahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Soudy. Najua nimekuwa nikisumbuliwa na mastaa wengi wa kiume ila sipo tayari kuwa nao maana najua tabia zao,”anasema.
Anasema yeye ni mwepesi wa kuumia, hivyo amekuwa muoga kuwa na uhusiano na mastaa.

0 Comments: