Monday, July 30, 2012

Kashfa yawakumba wanandoa wa jinsia moja Zimbabwe

WANANDOA wa jinsia moja kutoka nchini Zimbabwe ambao walioana kwa ndoa iliyofanyika nchini Uingereza mwaka jana wameingia katika kashfa nzito baada ya video iliyosambaa nchini humo ikimwonyesha mmoja wao akimsaliti mwenzake.

Video hiyo ambayo iliwekwa katika tovuti ya mtandao wa kijamii wa You Tube ilichukuliwa katika nyumba wanayoishi wawili hao
Nicky Chigoba Chalenga na mpenzi shoga mwenzake Chido Chalenga.

Katika video hiyo Chido anaonekana kuwa na Brenda Muchi Soko ambaye ni dada wa DJ maarufu na mtangazaji nchini Zimbabwe Petro C Soko ambaye ni rafiki wa ndoa yao. Lakini kwa wakati huu rafiki huyu ameonekana katika kitanda cha mashoga hao na Chido ambaye ni mwanandoa wa Nicky.

"Brenda unafanya nini katika nyumba yangu, na Chido katika kitanda changu? nini kinaendelea hapa?" Nicky aliwauliza wawili hao.

Chido aliduwaa, huku Brenda ambaye anaishi na mume wake karibu na nyumba hiyo akiwa hana la kufanya, Nicky alimaliza kutengeneza video hiyo na baadaye alienda kuiweka wazi katika mtandao huo wa kijamii.

Kitendo hicho cha kufadhaisha kimemweka Dj Soko katika wakati mgumu huku dada yake Brenda akijitahidi kujisafisha katika mtandao wa kijamii wa Facebook kupitia kundi la 'Dandaro NemaGirls' ambapo amewaomba msamaha wanakundi wenzake na kuwaomba wamvumilie katika kipindi hiki.

Bado haijajulikana wazi hatma ya mashoga hao, lakini Nicky mume wa Chido ameendelea kuongea maneno mbalimbali kupitia mtandao wa kijamii yakiashiria kutoa msamaha kwa shoga mwenzake huyo.

Nicky na Chido ni miongoni mwa wasagaji wa kwanza wa Zimbabwe kuamua kufunga ndoa na kujitangaza hadharani na kutambulika katika umma. Wawili hawa wana mtoto wao wa pamoja waliomuasili,

0 Comments: