Tuesday, August 15, 2017

Fella:Sina tatizo na Kiba...mbona mwanangu tu

SAID Fella ameamua kutoa la moyoni kuwa yupo tayari kufanya kazi na msanii Ali Kiba a.k.a King Kiba licha ya muda mrefu amekuwa akimsimamia Nasib Abdul ‘Diamond Platnumz’
Ametoa kauli hiyo ili kujibu wale ambao wamekuwa wakiamini Fella hawezi kufanya kazi na Kiba kwasababu ya kuwa Diamond ambapo anaeleza wazi hana tatizo lolote na yupo tayari kufanya kazi naye.
Akizungumza jijini Dar es Salaam Fella anasema “Sijawahi kusema sifanyi kazi na mtu yeyote, Ali Kiba ni mwanangu wa dhahabu japokuwa wanasema chawa, basi chawa aje vizuri.
“Kwa sababu mimi ndiye meneja wa kwanza katika muziki huu sina pingamizi kuwa nitafanya kazi na mtu niogope kufanya kazi na mtu,”anasema Fella.
Anafafanua yeye ndio Mkubwa na wanae, kwa hiyo Alikiba naye ni mwanaye na hata siku moja hawajawahi kugombana.

0 Comments: