Tuesday, August 23, 2011

TAARIFA RASMI KUHUSU HUSSEIN MACHOZI KUREJEA TETEMESHA




Hello mdau,

Hii ni taarifa rasmi kwa media na wadau wote kuhusiana na HUSSEIN MACHOZI kurejea katika familia ya TETEMESHA RECORDZ, iliyomtengeneza na kumkuza kimuziki mpaka hapo alipo toka mwaka 2007.

Kumekuwa na taarifa nyingi hapo katikati lakini hii ndio taarifa rasmi na ya kweli kuwa yalitokea matatizo kidogo mwaka jana (2010) mwanzoni, yaliyotokana na Hussein kukiuka baadhi ya masharti ya mkataba wake na Tetemesha, yaliyopelekea uongozi kuamua kusitisha kwa muda mkataba wake ili kumpa nafasi ya kupewa nguvu msanii mwingine aliyekuwa ndio anaaza kutambuulishwa mwaka jana anayefahamika kama SAGNA. Baada ya kumtambulisha vizuri Sagna, mwaka huu pia Tetemesha tumeweza kumtambulisha msanii mwingine wa tatu aitwaye C-SIR MADINI.

Sasa tumeona ni wakati muafaka wa kumrudisha Hussein Machozi rasmi ndani ya Tetemesha baada ya kukaa nae chini na kufanya makubaliano mapya na kusaini mkataba mwingine toka katikati ya mwaka huu, isipokuwa tumechelewa kuwapa taarifa kwasababu tulikuwa tunaweka kwanza mambo kadhaa sawa.


NEW SONG:

Hussein Machozi akiwa chini ya Tetemesha Entertainment ameshaanza kurekodi baadhi ya nyimbo mpya zitakazotoka mwaka ujao 2012, lakini kwa sasa tunautambulisha wimbo wake ambao ni REMIX ya wimbo alioutoa mwaka jana unaitwa “UNANIFAA”.

Katika version ya mwanzo ya wimbo huo aliimba peke yake, lakini katika remix hii amewashirikisha wasanii wenzake wa Tetemesha ambao ni C-sir Madini na Sagna.

Unanifaa remix imeandikwa na Hussein mwenyewe verse yake na chorus, na verse za Sagna na C-sir zimeandikwa na mwandishi rasmi wa Tetemesha anaitwa JOSEFLY kwa kushirikiana na Kid Bwoy.

Version ya mwanzo ya wimbo huo ilifanyika Akhenato Records chini ya Lil Ghetto. Remix beat imefanywa na Amba, na vilivyosalia vyote vimefanyika Tetemesha Recordz.


CREDITS:

Artists: HUSSEIN MACHOZI FT. C-SIR MADINI & SAGNA

Song title: UNANIFAA (REMIX)

Written by: Verse-1: JOSEFLY, Verse-2 & Chorus: HUSSEIN MACHOZI, Verse-3: JOSEFLY & KID BWOY

Produced by: AMBA for TETEMESHA RECORDZ 2011

Vocals Recorded by: KID BWOY

Mixed by: KID BWOY

Studio: TETEMESHA RECORDZ (Mwanza)


CONTACTS:

Hussein Machozi 0718 877728

Kid Bwoy 0713 131073

Thanx for the support.

Sandu George. (Kid Bwoy)

C.E.O Tetemesha Entertainment.



LYRICS

"UNANIFAA (REMIX)" LYRICS by HUSSEIN MACHOZI FT. C-SIR MADINI & SAGNA


Song title: UNANIFAA (REMIX)
Artists: HUSSEIN MACHOZI FT. C-SIR MADINI & SAGNA
Song written by: HUSSEIN MACHOZI, JOSEFLY & KID BWOY
arranged by: KID BWOY
Produced by: AMBA & KID BWOY
Mixed by: KID BWOY
Studio: TETEMESHA RECORDZ
AUGUST 2011


Verse 1 (C-sir Madini):

Bado mi najiuliza alobatiza hisia za moyo jina mapenzi weweee,
kwani mi lanitatiza mpaka najikuna pasipowasha kisa wewee,
nilipokuwa mi mdogo nilipohisi njaa, niliweza kutamka mama mi nanjaa,
ila leo mi mkubwa nahisi mapenzi, tatizo moja kusema neno nakupenda,
iliniuma sanaaa, uliponieleza hisia zako kwa yuleeee,
ukaniomba ushauri wa bure, wakati nami nakupenda zaidi ya yuleee eeh heee,
kweli inaniuma sanaaa, kuona tayari umeanza mapenzi na yuleee,
na nilivyo bwege wa karne, mimi mwenyewe niliekushauri umkubaliee eeh hee,

Bridge:(C-sir):
C-sir nimependa, ila nashindwa kukutamkiaaa,
nabaki tazama, nakula kwa hisiaaa,
C-sir nimependa, ila nashindwa kukutamkiaaa,
nabaki tazama, nakula kwa hisiaaa baby,

Chorus (Hussein Machozi):
Kama sifaaa, zote nakupaa,
ama kwa hakika, unanifaa,
Kama sifaaa, zote nakupaa,
ama kwa hakika, unanifaa,


Verse-2 (Hussein Machozi):

Hisia zangu zinanitesa hadi nakondaaa,
mbaya zaidi napokuona moyo unadundaaa,
natamani ungejua nini nawazaaa,
labda ingekuwa rahisi mi kukupataaaa,
taswira ya sura yako inanijiaaa,
ndo maana siachi kuwaza kila napokwendaaa,


Bridge:(Hussein):
Nahisi napenda, ila nashindwa kukwambiaaa,
nabaki tazama, nakula kwa kuonaaa,
Nahisi napenda, ila nashindwa kukwambiaaa,
nabaki tazama, nakula kwa kuona eeei eeh,


Chorus (HUSSEIN MACHOZI):
Kama sifaaa, zote nakupaa,
ama kwa hakika, unanifaa,
Kama sifaaa, zote nakupaa,
ama kwa hakika, unanifaa,


Verse-3 (Sajna):

Wingi wa nyuki kwa mzinga hauongezi utamu wa asali,
japo mi fundi wa maneno lakini kwako sina hali,
mara ya kwanza kwenye facebook, sajna sajna naomba urafiki,
sina hiyana mimi mtu wa watu, nawe ukawa wangu rafiki,
kimoyomoyo mi nasema nakupenda ah ah,
kwa sauti nashindwa kutamka,
moyo wangu hauwezi acha kukupenda ah ah,
mdomo unashindwa kutamka,
nimetumia lugha ya vitendo lakini nimepata zero,
nimejituma kuonesha upendo lakini huoni mi hero,

Bridge:(Sajna)
oooh oh kama sifaa, zote nakupa mama, wewe unanifaa wewe unanifaa sana mimi,
oooh oh kama sifaa, zote nakupa mama, wewe unanifaa wewe unanifaa sana mimi,


Chorus (Hussein Machozi & Sajna):
Kama sifaaa, zote nakupaa,
ama kwa hakika, unanifaa,
Kama sifaaa, zote nakupaa,
ama kwa hakika, unanifaa,

END


0 Comments: