Friday, January 13, 2017

Dully auzungumzia wimbo wa Darassa

MSANII wa Bongo Fleva Dully Sykes ameibuka na kueleza kuwa wimbo wa Muziki wa msanii Darassa hauna ujumbe wa aina yoyote ila zina bahati ya kuhit.
Akizunguma siku za karibuni kwenye kipindi cha Planet Bongo cha EA Radio, Dullya anasema wimbo huo wa Darassa hauna ujumbe wowote kila umejaa majigambo na kujisifu.

“Nyimbo za aina hiyo ndizo hupendwa na watanzania walio wengi na iwapo angeamua kuimba wimbo wenye ujumbe wa maendeleo usingependwa,”anasema.
Dully aliamua kuuzungumzia wimbo wa Darassa wakati anaelezea mikakati yake kwa mwaka huu baada ya mwaka 2016 kufanikiwa kutamba na wimbo wake wa Inde.
“Kwani wimbo wa Darassa una ujumbe gani? sio Simba , Sio Chui, huko ni kujisifu maana wabongo ukiwaimbia twende tukalime au tufanye kazi ujue wimbo hautapendwa,”anasema Dully.


0 Comments: